Job 27:1-6
Ayubu Anadumisha Uadilifu Wake
1 aNdipo Ayubu akaendelea na hoja yake, akasema:2 b“Hakika kama Mungu aishivyo, aliyeninyima haki yangu,
Mwenyezi ambaye amenifanya
nionje uchungu wa nafsi,
3 ckwa muda wote nitakaokuwa na uhai ndani yangu,
nayo pumzi ya Mungu ikiwa puani mwangu,
4 dmidomo yangu haitanena uovu,
wala ulimi wangu hautatamka udanganyifu.
5 eSitakubaliana nanyi kabisa kuwa mko sahihi;
hadi nife, sitakana uadilifu wangu.
6 fNitadumisha haki yangu wala sitaiacha;
dhamiri yangu haitanisuta muda wote ninaoishi.
Copyright information for
SwhKC